Front page

MATANGAZO

KARIBU

Monday, April 15, 2013

JK:Watanzania watumie fursa zilizopo kuendeleza nchi

Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete
 
Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete
 

 
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania amesema kuwa, wananchi wanapaswa kutumia fursa za kiuchumi zilizoko ili kulisukuma mbele gurudumu la maendeleo ya nchi yao. Akizungumza wakati wa kuzindua barabara mpya ya Tanga-Horohoro yenye urefu wa kilometa 65, Rais Kikwete amesema kuweko miundombinu bora ni wenzo muhimu katika ukuaji wa uchumi. 

Amewataka Watanzania kutumia barabara zilizotengenezwa kuboresha maisha yao ya kila siku na vilevile kuboresha uchumi wa nchi. Kiongozi huyo ameahidi kwamba serikali yake itaendeleza sera ya kuboresha miundombinu ili ifikapo mwaka 2015, awe ametekeleza ahadi yake aliyoitoa ya kujenga barabara za lami zenye urefu wa zaidi ya kilomita 11,000. 

Baadhi ya mashirika ya kijamii yamejibu mwito wa rais kwa kumtaka ashughulikie suala la ulaji rushwa kwanza ndani ya serikali yake iwapo kweli ana nia ya kuboresha uchumi wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment