Front page

MATANGAZO

KARIBU

Thursday, December 12, 2013

MIKOPO TOKA SACCOS



NA REHEMA MBANDO-MOSHI
 
Chama cha kuweka na kukopa cha Muungano Kikavuchini (SACCOS) kimefanikiwa kutoa mikopo ya aina mbalimbali kwa wanachama wake ya jumla ya shilingi milioni 609 kwa kipindi cha Januari   mwaka huu hadi desemba mwaka huu.

Chama hicho kilichopo katika kata ya Machame Weruweru wilayani Hai   kinachohudumiwa wananchi wa Wilaya tatu  za mkoa wa Manyara na Kilimanjaro kimefanikiwa  kimefanikiwa kutoa mikopo hiyo baada ya kutoa elimu  kwa wanachama wake umuhimu wa kukosa katika Saccos.

Akitoa taarifa hiyo katika mkutano mkuu wa mwaka wa Chama hicho katibu wa bodi Mary Tesha alisema katika kipindi cha Januari hadi desemba mwaka huu wameweza aina sita kwa wanachama ambapo wametoa jumla ya shilingi milioni 249  kwa ajili kilimo na shilingi milioni 70 kwa ajili ya shughuli za kijasiriamali.

Amefafanua kuwa kutokana na mafanikio hayo Chama hicho kimekusudia kutoa mikopo aina mbalimbali kwa wanachama wake katika mwaka 2014 ya jumla shilingi bilioni 1 ikiwemo ya kiklimo, biashara, dharura vifaa, kijamii  na chapchapu ambayo itawasaidia kuondoka na wimbi la umaskini
Mwenyekiti huyo amefafanunua kuwa wameweza kupatya mafanikio mengine tofauti na kutoa huduma kwa wanachama ni pamoja na kuwa na eneo la kujenga ofisi ndogo katika kijiji Kawaya pamoja na kununua matofali kwa ajili nya ujenzi ofisi ya SACCOS tawi la Chemchemu

No comments:

Post a Comment