Front page

MATANGAZO

KARIBU

Tuesday, December 31, 2013

MERU WAJIPANGA 2014

NA ONESMO LOI

ARUSHA

Halmashauri ya wilaya ya Meru mkoani Arusha imejipanga kwa mwaka 2014, kusambaza maji katika vijiji kumi pamoja na miradi wa   elimu na kilimo  miradi ambayo itatumia zaidi ya bilioni 6.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Meru STEAS KAGENZI,amesema kuwa mipango ya upelekaji wa maji umeanza katika maeneo mengi hiyo ushirikiano na wananchi katika kufanikisha hilo ndio jambo kubwa ambalo halmashauri inalitarajia.
Aidha amesema kuwa, utaratibu  wa mpango wa elimu ni miongoni mwa mambo ambayo  halmashauri imejiwekea kwa mwaka 2014. Akifafanua hali ya kilimo wilayani meru mkoani hapa amewata wakulima kujaribu kilimo cha mtama hasa katika kata ya maroroni , Mbuguni  na  Makiba ambazo zina kabiliwa na ukame.Kuhusu afya amesema mipango iko mbioni  kwa mwaka ujao kwani ni lengo la serikali kuboresha huduma ya afya kwa kiwango stahili .

No comments:

Post a Comment