Front page

MATANGAZO

KARIBU

Tuesday, December 31, 2013

40 wauawa Kongo

Majeshi ya usalama katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo yamewauwa kiasi wanamgambo 40 wenye silaha leo wakati mapigano makali yakitikisa wilaya mbali mbali za mji mkuu Kinshasa.Mapigano yalizuka katika uwanja wa kimataifa wa ndege na makao makuu ya jeshi , wakati polisi wamesema vijana wenye silaha waliwateka nyara waandishi habari kutoka kituo cha televisheni cha taifa RTNC. 
Msemaji wa serikali Lambert Mende PICHANI  ameliambia shirika la habari la AFP kuwa washambuliaji 16 wameuwawa katika uwanja wa ndege, 16 katika kituo cha jeshi cha Tshatshi na wengine wanane wameuwawa katika maeneo ya jengo la televisheni la RTNC.Madhumuni ya washambuliaji hao hayajafahamika ingawa kumekuwa na dhana nyingi kuhusiana nayo.

Hakuna raia ameripotiwa kuuwawa na pia hakuna mwanajeshi aliyeuwawa. Katika taarifa iliyosomwa katika televisheni , Mende amesema uvamizi huo ulikuwa na lengo la kuwatisha raia mjini Kinshasa. Mfanyakazi wa televisheni amesema kuwa watu waliowateka nyara wamedai kuwa ni wafuasi wa mchungaji Joseph Mukungubila Mutombo, mmoja kati ya wagombea wa kiti cha urais katika uchaguzi wa mwaka 2006 ambapo rais Joseph Kabila alishinda.

No comments:

Post a Comment