Karibu watu sabini wameuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa
kufuatia mlipuko mkubwa katika kiwanda cha mbolea katika jimbo la Texas
nchini Marekani.
Maafisa wa uokoaji wanasema kati ya watu 60 na 70 wamepoteza maisha katika mlipuko huo uliojiri katika mji wa West.
Idadi hiyo inatazamiwa kuongezeka. Sababu ya mlipuko huo bado haijajulikana. Moto unaripotiwa kuenea katika majengo kadhaa ambapo zahanati moja imeteketea kabisa na shule ya msingi kupata uharibifu mkubwa. Aidha kufuatia mlipuko huo umeme umekatika katika maeneo kadhaa mjini humo.
Watu wengi wanaripotiwa kuukimbia mji huo kutokana na hofu ya kujiri mlipuko mkubwa wa mada za kemikali katika kiwanda hicho cha mbolea. Mlipuko huo umetokea siku chache tu baada ya watu watatu kupoteza maisha kufuatia mlipuko katika kituo cha kumalizia mbio za Marathoni mjini Boston.
Maafisa wa uokoaji wanasema kati ya watu 60 na 70 wamepoteza maisha katika mlipuko huo uliojiri katika mji wa West.
Idadi hiyo inatazamiwa kuongezeka. Sababu ya mlipuko huo bado haijajulikana. Moto unaripotiwa kuenea katika majengo kadhaa ambapo zahanati moja imeteketea kabisa na shule ya msingi kupata uharibifu mkubwa. Aidha kufuatia mlipuko huo umeme umekatika katika maeneo kadhaa mjini humo.
Watu wengi wanaripotiwa kuukimbia mji huo kutokana na hofu ya kujiri mlipuko mkubwa wa mada za kemikali katika kiwanda hicho cha mbolea. Mlipuko huo umetokea siku chache tu baada ya watu watatu kupoteza maisha kufuatia mlipuko katika kituo cha kumalizia mbio za Marathoni mjini Boston.
No comments:
Post a Comment