Umoja wa Mataifa
umetangaza kuwa, utatuma kikosi cha askari 3,069 mashariki mwa Jamhuri
ya Kidemokrasia ya Kongo kwa shabaha ya kwenda kupambana na makundi ya
waasi katika eneo hilo.
Madnodje Mounoubai, Msemaji wa vikosi vya
kusimamia amani vya Umoja wa Mataifa huko Kongo DRC ametangaza kuwa,
idadi hiyo ni rasmi na kwamba, askari hao wataungana na vikosi vingine
vya umoja huo vilivyoko Kongo.
Afrika Kusini, Tanzania na Malawi
zimetajwa kuwa ndizo zitakazounda kikosi hicho cha kimataifa. Hata hivyo
hivi karibuni Afrika Kusini ilisema kuwa haina mpango wa kutuma majeshi
yake mashariki mwa Kongo. Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa,
kikosi hicho cha kimataifa kitaongozwa na jenerali kutoka Tanzania
ambaye hakumtaja jina lake.
Hatua ya kutumwa kikosi cha Umoja wa Mataifa
mashariki mwa Kongo ni kutekeleza azimio la Baraza la Usalama la mwezi
Machi uliopita ambalo linataka kupelekwa kikosi cha kimataifa katika
maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo ili kupambana na makundi ya waasi.
Wakati huo huo, waasi wa M23 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
wameionya serikali ya Tanzania na kuitaka iachane na uamuzi wake wa
kutaka kutuma majeshi yake Kongo DRC.
source.....idhaa ya Tehran
No comments:
Post a Comment