Front page

MATANGAZO

KARIBU

Monday, April 15, 2013

Msongamano wa magari chanzo cha maradhi ya akili, moyo

Msongamano wa magari jijini Dar es Salaam

 


makala maalum


Wakati tatizo sugu la foleni likiendelea kuwaumiza wakazi wa Dar es Salaam na viunga vyake, utafiti mpya umebaini kuwa watu wanaokaa katika foleni mara kwa mara na kwa muda mrefu huweza kupata maradhi ya akili.
Imebainika kuwa foleni huchangia kwa kiasi kikubwa kusababisha maradhi ya akili yanayoweza kujitokeza baada ya miaka kumi, pamoja na ugonjwa wa moyo.
Utafiti huo uliofanywa na Taasisi ya Saikolojia na Tabia za Watu ya nchini Marekani, umebainisha kuwa kukaa katika msongamano wa magari kwa muda mrefu, husababisha mtu kunong’ona au kulalama, hatimaye kutoa sauti kwa kubwa.

Matokeo ya utafiti huo uliofanywa pia na Mradi wa Maendeleo wa Marekani (MDM), ulijumuisha wanaume na wanawake wenye miaka 25 na 74.
Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia(NCCR) aliwahi kusema kuwa tatizo la msongamano wa magari hulisababishia taifa hasara ya takriban Sh1.46 trilioni kwa mwaka.
Ilibainika kuwa matatizo ya akili huweza kusababishwa pia na changamoto katika maisha, ikiwemo kukerwa au kuudhiwa katika misongamano ya magari.
Utafiti huo pia uliungwa mkono na Mtaalamu wa Saikolojia wa Chuo Kikuu cha Dodoma Modester Kimonga, aliyesema kuwa kukaa kwenye foleni kwa muda mrefu husababisha hasira, hatimaye msongo wa mawazo.

source....Gazeti Mwananchi

No comments:

Post a Comment