Front page

MATANGAZO

KARIBU

Saturday, December 28, 2013

Igad haitokubali kupinduliwa serikali ya Sudan Kusini

Nchi zilizo jirani na Sudan Kusini zimesema haziwezi kuruhusu vita vya kutaka kuiondowa  kwa nguvu madarakani serikali ya rais Salva Kiir  iliyochaguliwa kwa njia za kidemokrasia.Hatuwa hiyo imekuja baada ya  takriban wiki mbili za mapigano kati ya wanajeshi wa serikali na wale wanaomuunga mkono makamu wake wa zamani.Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta akizungumza katika mkutano maalum wa viongozi wa nchi za Jumuiya ya kiserikali ya ushirikiano wa Maendeleo mashariki mwa Afrika -IGAD  ametowa mwito kwa rais Kiir na makamo wake wa zamani Riek Machar  kutumia nafasi iliyopo na kuanzisha mazungumzo ya amani.Rais Kenyatta amesisitiza kwamba vita sio suluhisho la mgogoro katika taifa hilo changa.Mkutano huo wa IGAD unatarajiwa kuanzisha mpango wa kusaka maridhiano kati ya rais Kiir na mpinzani wake Riek Machar anayetuhumiwa kuanzisha jaribio la mapinduzi lililoshindwa na ambalo serikali imesema ndiyo chanzo cha  mapigano yanayoshuhudiwa sasa Sudan Kusini...DW SWAHILI

No comments:

Post a Comment