Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA ), Profesa
John Nkoma, akizungumza kwenye mkutano wa pamoja na viongozi wa Kampuni
za Simu kuhusu usajili wa laini za simu Dar es Salaam jana. Picha na
Rafael Lubava.
Dar es Salaam
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kisheria mtu anayetumia simu isiyosajiliwa akikamatwa anaweza kutozwa faini ya Sh500,000 au kwenda jela miezi sita.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kisheria mtu anayetumia simu isiyosajiliwa akikamatwa anaweza kutozwa faini ya Sh500,000 au kwenda jela miezi sita.
‘‘Kwa mujibu wa kifungu cha 131 cha sheria ya
mawasiliano mteja au muuzaji wa namba ya simu ambayo haijasajiliwa
atatozwa faini ya Sh500,000 au kifungo cha miezi mitatui’’ ilielezwa
jana.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma
alisema hayo alipokutana na wadau wa mawasiliano jijini hapa jana.
Profesa Nkoma alisema namba za simu ni lazima zisajiliwe kwa mujibu wa
sheria ya mawasiliano ya elekroniki na Posta (EPOCA) ya mwaka 2010.
Ufafanuzi wa TCRA umekuja baada ya kuwapo
malalamiko ya watu wa kada mbalimbali kwamba mawasiliano yao ya simu
yanaingiliwa na kuchapishwa katika vyombo vya habari. Katika maelezo yake ya jana, Pofesa Nkoma alisema
kwa mujibu wa kifungu cha 130 cha sheria ya EPOCA ya mwaka 2010, mtu
ambaye atauza au kutoa namba za simu bila ya kusajiliwa atachukuliwa
hatua za kisheria na adhabu yake ni faini ya Sh3 milioni na kifungo cha
miezi 12.
No comments:
Post a Comment