MWANAMKE ANAYEDAIWA KUFARIKI MIAKA MITANO ILIYOPITA |
Geita:
Mji wa Geita na maeneo ya jirani juzi ulikumbwa na taharuki ya aina yake, pale mwanamke ambaye anadaiwa kwamba alifariki miaka mitano iliyopita alipoonekana akiwa hai katika eneo la Kasamwa.
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki
Februari 28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika
Kijiji cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa
ameketi nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi
Kasamwa.
Aliyekuwa wa kwanza kumwona Flora ni mdogo wake
aitwaye Monica Onesmo ambaye baada ya kuamka saa 11:00 alfajiri nyumbani
kwa dada yake, alimwona mwanamke aliyekuwa ameketi nje ya nyumba hiyo,
lakini alimfananisha mwanamama huyo na marehemu dada yake.
“Baada ya kumwona nilimwita mtoto wake tunayekaa
naye na nikampigia simu dada (Monica) ambaye alikuwa amelala chumba
kingine nikamwambia kwamba nimeamka na kumkuta mwanamke amekaa hapa nje,
lakini kila nikimwangalia anafanana na marehemu dada yetu,”alisema
Jubili na kuongeza kwamba alipowaita wote walitoka nje.
Alisema mtoto wa Flora (marehemu anayedaiwa
kufufuka) anaitwa Rebeka Elisha (16) na kwamba walimchukua tangu 2008
wakati mama yake huyo alipofariki dunia katika Hospitali ya Geita ambako
alikuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa ini.
Rebeka ambaye ni mtoto wa nne wa Flora alisema:
“Mama mdogo alituita sisi tulikuwa tumelala akasema kwamba nje kuna
mwanamke ambaye anafanana na marehemu mama yetu, ndipo na sisi tukatoka
na kweli kumwangalia alikuwa ni yeye kabisa.”
SOURCE....MWANANCHI
SOURCE....MWANANCHI
No comments:
Post a Comment