Front page

MATANGAZO

KARIBU

Wednesday, March 27, 2013

William Hague amzungumzia Ntaganda

Waziri wa nchi za nje wa Uingereza Wiiliam Hague
Willium Hague
Wakati Bosco Ntaganda akitarajiwa kusomewa mashtaka yake katika mahakama ya ICC, waziri wa mashauri ya kigeni wa Uingereza, amesema hiyo ni hatua moja muhimu iliyopigwa kueleka mustakabali wa usalama mashariki mwa DRC


William Hague ambaye anafanya ziara kwenye eneo la maziwa makuu akiwa pamoja na mjumbe maalum wa shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR Angelina Jolie, amesema hatua ya Bosco Ntaganda kupelekwa ICC na mwisho kufikishwa kizimbani ni moja ya mafanikio makubwa ambayo nchi za kikanda zimeweza kuyapata kwa kipindi kigumu cha usalama mdogo kwenye kanda ya maziwa makuu.
Mbabe wa kivita Bosco Ntaganda Mbabe wa kivita Bosco Ntaganda
Hague amesema Rwanda imekuwa na mchango mkubwa kwenye mchakato huo ambao pengine unaweza kuiletea tija baadaye. "Hii ni moja ya mafanikio yaliyofikiwa na eneo zima, mathalan kukamatwa na kupelekwa Hague kwa Jenerali Bosco Ntaganda tunakaribisha maendeleo haya yote yaliyopatikana kwa kipindi kigumu. Lakini nisema tu kwamba Rwanda imekuwa na mchango mkubwa kwenye michakato hii yote." Alisema William Hague.

SOURCE DW

No comments:

Post a Comment